Monday, 10 February 2014

Ona Mchezo wa Mtandaoni Ulivyochukua Maisha ya Kijana Richard

"Nataka kuwashinda wengine wote", ndiyo yalikuwa maneno ya mwisho ya Isaac Richardson kijana mdogo mwenye umri wa miaka 20 aliyejiingiza katika shindano katika mtandano ikiwa ni shinikizo la marafiki, lililomtaka anywe mchanganyiko wa pombe kali ikiwa ni pamoja na mvinyo na bia.

Mchezo huu ujulikanao kama NekNomination uliopo Facebook, ni mchezo wa kunywa pombe kali, ambao vijana tofauti hutuma picha za video katika mitandao wakionyesha au wakifanya tambo ya michangayiko mbali mbali ambayo wameweza kuinywa. Vijana hawa wanakunywa michanganyiko ya ajabu ajabu ya pombe halafu wanawataka wenzao kwingine duniani wafanye zaidi ya wao kama wataweza.

Kijana Isaac Richardson ambaye bni muhudumu wa hote;li ya kifahari huko Uingereza aliwaambia wenzake anataka awashinde wengine wote waliowahi kushiriki mchezo huo.

Isaac amekuwa muingereza wa kwanza kufariki katika mchezo huo, huku kukiwa na taarifa za wengine wawili kufariki nchini Ireland kwa mchezo wa aina hiyo.

Muhudumu huyu wa hoteli
alipoteza fahamu dakika chache baadaya kunywa mchanganyiko huo na alipofikishwa hospitali alikwisha fariki dunia.

Mchezo huu ulianza nchini Australia mwezi uliopita sasa umesambaa kote duniani.
Maelfu ya vijana sasa Ulaya wanafanya majaribio ya aina hii kwanzia iliyo hatari zaidi mpaka inayotia kinyaa.




Mama mzazi wa Richard alishikwa na mfadhaiko wa ajabua laiposikia habari z amwanae kufariki dunia kiasi kwamba alishindwa kuzungumza.

Wazazi, walezi pamoja na makundi ya jamii Ulaya yameutaka mtandao wa kijamii wa Facebook kufutilia mabali mchezo huo kwani unapa mshawashawa viajna wa kutaka kujiingiza na kushiriki na pale mshindi anapotafutwa, mtu anakuwa na uwezo wa kujaribu jambo lolote.

Wazungu wanasema Curiousity Killed the Cat.

Hata kama ni kwa nchi Iliyo endelea....Ivi kweli kuna haja ya kufanya mambo kama haya?...


No comments:

Post a Comment