Tatto Mpyaaa ya Chameleone ... Ona alichochora...

0
Jose Chameleone, Staa wa muziki wa nchini Uganda katika kuonyesha upendo mkubwa alionao kwa mke wake Daniella, ameamua kujichora tattoo ya mke wake huyu katika shingo yake.

 Mbali na kusherehekea sikukuu ya wapendanao, Chameleone ambaye tayari ana tattoo za majina ya watoto wake wote katika mkono wake, amefanya hivi katika kum
thibitishia mama watoto wake kuwa, mbali na watoto wake, yeye pia ni mtu mwingine mwenye nafasi kubwa katika moyo wake.

0 comments: