NTAGANDA HAKUWA NA "OPTION" NDO MAANA ALIJISALIMISHA....

0
Kiongozi wa waasi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Bosco Ntaganda ambaye alikuwa akiogopewa mno anafikishwa mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), hii leo.

Muasi huyo ambaye alishangaza Marekani mwaka jana baada kujisalimisha kwenye Ubalozi wa Marekani nchini Rwanda, sasa anakabiliwa na makosa kadhaa yakiwemo ya ubakaji, mauaji na kutumia askari watoto.

Majaji wa Mahakama hiyo iliyopo The Hague, Uholanzi wanasiku 60
za kuamua iwapo Ntaganda anakesi ya kujibu, baada ya kuisikiliza shauri lake kwa mara ya kwanza hii leo.

Ntaganda ambaye alipewa jina la “The Terminator” alikuwa ndie muanzilishi wa kikundi cha waasi cha M23, ambacho kilisambaratishwa na vikosi vya Umoja wa Mataifa Novemba mwaka jana.

Ntaganda alikuwa sehemu ya Umoja wa wazalendo waasi wa kundi liloongozwa naThomas Lubanga ambaye mwishoni mwa mwaka jana alikuiwa mtu pekee aliyetiwa hatiani an ICC.

Mashariki mwa nchi ya kidemokrasia ya Kongo, kumekuwepo na miongo miwili ya ghasia zilizotokana na itikadi za kikabila ambapo makabila hayo yalikuwa yakipigania kutawala sehemu hiyo yenye madini ya thamani.

Ghasia hizo zilianza pale ambapo kundi la wahutu lilituhumiw akuhusiak moja kwa moja na ghasia na mauaji ya halaiki iliyotokea mwaka 1994. Kama tu wale walioitawala Rwanda kwanzia mauaji yale ya kirambi Generali Ntaganda ni Mtutsi.

Makundi ya haki za binadamu yalisherehekea Generali Gen Ntaganda's alipojisalimisha, kama ushindi wa mahamaka na sheria ya kiamataifa na pia ushindi kwa awaathirika wa vita.

Hata hivyo wadadisi wa kisiasa wanasema kujisalimisha kwake ni kama faid akwake kwani asinge jisalimisha angeuwawa, hivyo hii ni kama njia yake ya kubaki hai hata kama atafungwa.


0 comments: