MADAKTARI KENYA WAGOMA... WATAKA WAGONJWA WATAFUTE HUDUMA KWINGINE....
0
Umoja wa madakaktari na wauguzi nchini
Kenya umeita mgomo wa kitaifa kwa wanataaluma hao kufuatia kushindwa
kuafikiana na Serikali katika mazungumzo yaliyopangwa.
Katibu wa Chama cha Madaktari,
Wafamasia na Madaktari wa Meno, Sultani Matendechere ametangaza kuwa
mgomo huo utaanza usiku wa kuamkia leo katika hospitali zote za umma,
hivyo wagonmjwa watafute njia mbadala za kupatiwa matibabu.
Watumishi hao wa afya wanapinga hatua
ya serikali kuhamishia huduma za afya ikiwemo malipo ya mishahara yao
kuwa chini ya kaunti, badala ya serikali kuu yenyewe. Kaunti ni
mgawanyiko wa Nchi Mfano Kwa anzania tuna Mikoa, Lakini Kenya Zipo
Kaunti nchini Nyingine yapo Majimbo.
Wafanyakazi hao katika sekta ya afya,
wajumbe kutoka serikali za kaunti na serikali kuu walitumia takribani
siku nzima jana katika kujadili matatizo yao ilikuepusha mgomo wa
aina hii. Hata hivyo hawakufikia muafaka baada ya wafanyakazi hao
kuapa kuingia katika mgomo iwapo matakwa yao hayatotiliwa maanani.
Kwa muda mrefu kwanzia kuanzishwa kwa
mfumo wa kutoa madaraka kwa Kaunti hizi, Madaktari na wafanyakazi
wengine katika sekta ya afya wamekataa sekta hiyo kuwa chini ya
Majimbo yaani Kaunti badala yake wanataka sekta hiyo iendelee kuwa
chini ya serikali kuu.
Watu wengi nchini Kenya wamekuwa
wakipinga mfumo huu wenyewe wakiuita Devolution kwa sababu
mbalimbali. Katika mfumo huu itakuwa kwamba Kaunti hizi ndizo
zinzowalipa na kuendesha shughuli zoote za sekta. Kwa maneno mengine
Uwezo wa kaunti kifedha ndiyo utakaoamua ni kwa jinsi gani sekta
inaendeshwa. Madaktari wanahofu kuwa, Iwapo Kaunti kama ya Nairobi
ndiyo yenye kipato zaidi na nyingine siyo, basi hii italipa
wafanyakazi wake vizuri zaidi ya nyingine. Usawa, umakini utapotea
katika sekta.
Mwenyekiti wa Asasi ya Wauguzi ya Kenya
Bw. Nyaim Opot amesema kuwa mambo yahusuyo mafunzo, na taaluma nyeti
hayapaswi kuwekwa chini ya Kaunti. Ni mambho yakushughulikiwa na
serikali kuu. Hata hivyo awali asasi hii ilitoa muda wa wiki mbili wa
kurekebishiwa madai yao vinginevyo wataingia katika mgomo na wiki
hizo mbili ziliisha jana. Hivyo leo Wauguzi katika hospitali za umma
wapo katika mgomo.
Tukumbuke kuwa, Ni kipindi kifupi
kimepita tangu ipitishwe kura ya maoni kwa wananchi wa Kenya ya kuona
ni wangapi wanaafiki Mfumo huu wa uendeshwaji wa shughuli. Katika
kura hiyo, Mfumo huu wa kuzipa Kaunti madaraka ulipitishwa. Unaweza
kushangaa iweje sasa kuwepo malalamiko ya aina hii? Tutafakari
Waafrika Kura zetu ni za kushinikizwa? Au humaanisha yaleeeee
tunayoyataka?