 |
| Vladimir Putin Raqis wa Urusi |
Kuna msemo usemao kuwa wa kwanza si
kazi.. Kazi kubaki wakwanza. Hili limemsibu Rais Barack Obama wa Marekani baada ya
Rais wa Urusi Vladimir Putin kutajwa kuwa mtu mwenye nguvu na
ushawishi zaidi duniani kupitia jarida la Marekani la Forbes.
Putin amempiku Rais Barack Obama ambaye
kwa sasa anashikilia nafasi ya pili katika orodha hiyo.
Habari kutokana na Jarida hilo
zinaeleza kuwa Obama amekumbwa na anguko hili mapemo isivyo tarajiwa huku
Putin akionesha uwezo wake mkubwa wa kukabiliana na mambo mbalimbali
ndani na nje ya nchi.
Hii ni kwa mara ya kwanza kwa miaka
mitatu ambapo Rais Obama ameangushwa kufikia nafasi ya pili katika
Orodha ambayo hutolewa na Jarida hili la Forbes.
 |
| Barack Obama Rais wa Marekani |
Hali hii imehusishwa na mshikemshike
kati ya Marekani na Urusi katika Vita nchini Syria.
Rais Putin ambaye amekuwa akizitawala
siasa za Urusi kwa muda wa miaka 12 sasa, alichaguliwa tena kama Rais
wa nchi hiyo Mwaka jana mwezi machi.
Read More