WABUNGE WAKENYA NAFASI YA PILII KWA MALIPO YA JUU DUNIANI...

0
 
Wabunge wa bunge la Kenya wametajwa kuwa wapili katik aorodha ya wabunge wanaolipwa zaidi duniani, wakiwapiku wenzao kutoka nchini zilizoendelea zaidi duniani kama Marekani, Uingereza na Japan.

Utafiti uliofanywa na Mamlaka huru ya Viwango kwa Mabunge ya Uingereza(IPSA) ikishirikiana na Shirika la fedha duniani (IMF) umeonesha kuwa wabunge nchini kenya wanalipwa mara 220 ya pato la taifa la sh. Elfu 84,624. Kwa mt mmoja mmoja kwa mwaka.


Wanasiasa hawa wanapata mshahara wa Shs za Kenya Mill 90 za Tanzania huku pato la taifa la nchi hiyo likiwa chini ukilinganisha na nchi nyingine tajiri. Hii inaweza kuelezwa kuwa Wanbunge wanalipwa fedha nyingi sana.

Hata hivyo, wabunge hawa 416, wakiwemo wabunge wa kawaida 349, na wale wa Senate(bunge la juu) 67, wanapata asilimia 54% chini ya wenzao wa nchini Nigeriawanaopata jumla ya Shs Mill. 16.5 za Kenya takriban Dola 189,500

Malipo haya makubwa yameonekana kuharibu malipo ya wafanyakazi wa seriklai katika ofisi za Umma ambapo kima cha chini cha Mshahara kwa wafanyakazi ni Shs 85,790. kwa mwezi.

Riopoti hiyo inaonyesha kuwa, wabunge wamabunge manne kati ya matano wapo Afrika. Wakiongozwa na Nigeria, ikifuata Kenya, Ghana, Indonesia na Afrika ya Kusini.

Wabunge wa Uingereza wanapata kiasi cha Shs Mill. 91 kwa mwaka, wenzao wa marekani wakipata Mill. 15.1. Kwa marekani hii ni Asilimia 3.7 huku Uingereza ikiwa asilimia 2.7 ya pato la taifa.

0 comments: