WAANDISHI KENYA WAANDAMANA KWA AMANI...
0
Waandishi wa habari nchini Kenya leo
wameandamana kwa amani katika maeneo mbalimbali nchini humo kuonyesha
kukerwa na muswada wa sheria unaokandamiza uhuru wa vyombo vya
habari.
Wakati waandishi wakiandamana bunge la
Kenya mchana wa leo linmekutana kufanya mabadiliko katika baadhi ya
vipengele vya muswada huo uliopigiwa kelele mno na wadau wa habari.
Wajumbe wa kamati ya bunge wamekubali
kupunguza faini kwa mwandishi atakaekiuka maadili kutoka shilingi
laki tano za Kenya hadi shilingi laki moja, ambapo faini ya shs
milioni 20 kwa chombo cha habari, pia itapunguzwa.