MMILIKI WA "THE UGLIEST DOG" AOMBOLEZA KIFO CHAKE
0
Mbwa anayesadikiwa kuwa na sura mbaya
zaidi ya mbwa wote duniani amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 8
tu. Mbwa huyu ajulikanaye kwa jina la Elwood alijizulia umaarufu
mkubwa baada ya kuonekana kuwa mbwa mwenye sura mbaya zaidi. Mmiliki
wake Karen Quigley alithibitisha kifo cha kiumbe huyo mwenye sura ya
ajabu aliyewah kushinda tuzo mwaka 2007 amefariki dunia mwishoni mwa
wiki.
Mmiliki huyu mwenye umri wa miaka
52ambaye alizongwa na machozi alipomzungumzia mbwa wake alisema
amesikitishwa sana na kifo hicho kwani kilikuwa cha ghafla sana na
alifia mikononi mwake.
Mwanamke huyu alimnunua mbwa Elwood kutoka kwa
mmiliki wake wazamani mnamo mwaka 2006 baada ya mmiliki huyo kutaka
kumuua kwani alionekana kuwa na sura mbaya hivyo alishindwa kufanya
biashara.
Baada ya Elwood kufanikiwa kushinda
tuzo ya mbwa mwenye sura mbaya zaidi, alipata mamelfu ya mashabaiki
waliokuwa wakimtumia picha na barua mara kwa mara. Umaarufu wake pia ulipelekea kuandikwa kitabu kilichoitwa ‘Everyone Loves Elwood’.
Yaani kila mtu anampenda Elwood.