Rais Jakaya Kikwete ameongoza watanzania kuadhimisha siku ya ulemavu.
0
Tanzania
leo inaungana na nchi nyingine za Afrika Mashariki kuadhimisha siku
ya watu wenye ulemavu duniani ambapo Rais Jakaya Mrisho Kikwete
anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.
Kwa
mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa shirikisho la watu wenye ulemavu
nchini Tanzania Amon Anastaz maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika
katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Amesema
kauli mbiu ya siku hiyo ni ondosha vizuizi fungua milango kwa ajili
ya jamii jumuishi kwa wote.