JAGUAR sasa karibu na P Square, Radio& Weasel...
0
Msanii Charles Njagua Kanyi "Jaguar" anaonekana kutanua wigo wa Muziki wake kufika Afrika ya Magharibi na Kusini kupitia mkataba mpya wa
usambazaji kazi za muziki ambao amesaini na kampuni
ya MTech Kenya.
Jaguar kwa sasa yupo katika michongo ya kufanya kolabo
ya aina yake na msanii Ice Prince kutoka Nigeria.
Kampuni ambayo Jaguar
amesaini nayo mkataba tayari inafanya kazi na wasanii wengine wengi wakali
kama Wyre, Victoria Kimani, Ice Prince vile vile P Square kutoka
Nigeria, na Radio na Weasel wa Uganda.