Kesi ya Rwanda yenye UTATA, yasikilizwa Ufaransa

0

Miaka ishirini bada ya mauaji ya mauaji ya Kimbari nchini Rwanda, (Genocide), nchi ya ufaransa sasa imemfungulia mashtaka mtuhumiwa mmoja anayetuhumiwa kuhusika na mauaji ya takriban watu laki 8.

Aliyewahi kuwa mkuu wa kitengo cha kiintelijensia nchini Rwanda Bw. Pascal Simbikangwa amejisalimisha mahakamani hapo hiyo jana katika kesi ambayo imekuwa ikisubiriwa kwa hamu, huku mashahidi wakisafirishwa kutoka Rwanda kwenda kutoa ushahidi dhidi ya bwana huyo.

Bw. Pascal mwenye umri wa miaka 55, aliyepatwa na ukilema kwanzia mwaka 1986, anatuhumiwa kuhusika sio moja kwa moja na mauaji ya halaiki na uhalifu dhidi ya ubinadamu. Alikwisha pata kifungo katika jela ya ufaransa iliyopo katika kisiwa cha Mayotte mwaka 2008. hata hivyo wakili wa Bw. Pascal Simbikangwa anasema kuwa mteja wake anakataa tuhuma hizo iwapo atakutwa na hatia basi atatumikia kifungo cha Maisha Jela.

Kesi hii inasemekana ni ya utata kwani hakuna mashahidi wa moja kwa moja.

Maujai haya ya kimbari yalihusisha wanaharakati wa jamii ya wahutu waliolenga kuwauwa wale wa jamii ya watutsi katika miezi mitatu ya mauji mnamo mwaka 1994. Hata hivyo wale wahutu walioonekana kupingana na utaratibu waliathirika na ghasia zilizosababisha kuangushw akwa ndege aliokuwamo Rais wa Rwanda wa wakati huo Bw.Juvenal Habyarimana.

Bw. Simbikangwa Mtuhumiwa huyu aliachana na kazi za jeshi baada ya kupata ukilema hivyo kujiunga katika kitengo cha Intelijensia.

Wengi wa ndugu jamaa na marafiki wa walioathiriwa na mauaji hayo wamekuwa wakisubiri kwa hamu kusikilizwa kwa kwesi hii, huku wengi wa washitaki wakisema hawataki kulipiza kisasi bali wanataka haki itendeke.

Nchi ya ufaransa imeshutumiwa kuwa naugumu wa kuwatia hatiani watuhumiwa wa kesi hizi, ukilinganisha na nchini nyingine kama Ubeljiji, ziliwatia watuhumiwa hatiani mara moja.

Mabadiliko ya kisheria mnamo mwaka 1996, uliipa uwezo Rwanda kupeleka wananchi wake watuhumiwa wa kesi za mauaji haya kusikilizwa katika mahakama za Ufaransa. Ufaransa iliwahi kupigwa faini na mahakama ya ulaya ya haki za binadamu mnamo mwaka 2004 kwa tabia hii ya kuchelewesha kutolewa kwa haki.

Wadadisi wanadai kuwa hii hutokea kwasababu ya kukosa utayari wa kisiasa. Hata hivyo Rwanda iliwahi kuvunja mahusiano yake na ufaransa mwaka 2006 yaliyorejea tena miaka mitatu baadae.

Kesi hii ya Bwana Simbikangwa, ni hatua muhimu katika kuendelea kuweka msingi imara wa daraja madhubuti baina ya nchini hizi mbili. Hukumu ya kesi hii inategemewa kutolewa katikati ya mwezi machi mwaka huu.

0 comments: