HAS DEMOCRACY IN THAILAND FAILED OR IT IS JUST NOT THE SOLUTION...

0
Ghasia na maandamano ya upinzani nchini Thailand, yamechangia kuchafua hali ya utulivu na amani katika chaguzi kuu zilizofanyika nchini humo hapo jana.

Ghasia hizi zilipeleea kusitishwa kwa zoezi la kupiga kura katika sehemu za Bangkok na kusini mwa nchi hiyo. Hata hivyo maafisa wamedai kuwa takriban asilimia 89 ya vituo vyote vya kupigia kura vilifanya kazi kama kawaida.

Tume maalumu ya chaguzi ilisema kuwa ghasia hizo ziliwaathirri karibia watu mill. 6. Waziri mkuu wa nchini hiyo mwana mama Yingluck Shinawatra aliita chaguzi hizo akidhani zingemaliza ghasia za upinzani zilizoanza wii kadhaa zilizopita.

Japokuwa Chama chake kinakubalika sana nchini humo, na kinategemewa kushinda., changamoto kadhaa za kisheria na maelewano mabovu baina ya wanasiasa yanaweza kuleta mkanganyiko fulani. Baada kutangazwa kwa hali ya hatari nchini Thailand, maeneo kadhaa yamedhibitiwa huku kukiw an aulinzi wa kutosha.

Maafisa wa usalma wamesema kuwa, takriban askari 130,000 walitawanywa maeneo mbalimbali ya nchi hiyo hapo jana na wengine 12,000 kuwepo katika mji mkuu wa Bangkok.

Chaguzi hizi zilikuwa na mambo kadhaa yasiyo ya kawaida.
Kwanza Kampeni zilifanyika kidogo sana, pengine inaweza kusemekana hazikufanyika kabisa. Hakuna idadi kamili ya wapiga kura iliyotolewa. (kama walikurupuka)


Tofauti na chaguzi za awali zilizozoeleka kufanyika kwa amani, Chaguzi hizi zilifanyika katika ghasia zikidhaniwa kumaliza ghasia zilizopo. Hata hivyo kiongozi wa upinznaia Bw. Suthep Thaugsuban amesema itakuwa ngumu kwa serikali kutangaza matokeo kwani utata ni mwingi sana katika chaguzi hizi hasa ukizingatia sio wote waliotaka kupiga kura hiyo walifanikiwa.

Maandamno ya upinzani yalianza mwaka jana mwezi Novemba, baada ya serikali ya Thailand iliyopo chini ya waziri mkuu bi Yingluck kutaka kupitisha sheria ya msamaha ambayo ingemrudisha nchini Kaka yake Bw Thanksin ambaye amewahi kuwa waziri mkuu nchini humo wakati alikuwa akiishi uhamishoni. Bw huyu alitoroka nchini alipokuwa na kesi ya kujibu mwaka 2008 na inasemekana anaendesha nchi akiwa nje kwa mgongo wa mdogo wake mwana mama Yingluck.

Japo kuwa chama cha mama huyu kina wafuasi wengi, mkanganyiko wa vitambulisho vya kujiandiskisha kupiga kura vinaweza kumfanya asipate wabunge wengi safari hii, hivyo kukosa mamlaka ya kutosha juu ya Serikali. Chaguzi ndogo zinatarajiwa.

Wakati bi Yingliuck na chama chake wakiwa na kesi nyingi za kujibu mahakamani, wafuasi wa mwana mama huyu wanahofu, huenda



mahakama ikaingilia matokeo ya chaguzi hizi.

Chaguzi za jana zilikuwa na utofauti mkubwa sana na zile zilizopita miaka mitatu iliyopita, ambapo Bi Yingluck aliacha kazi yake nzuri aliokuw aakifanya kama mkurugenzi katik akampuni nak uingi akatik asiasa na kusababisha kushind akw akishindo kwa chama chake cha Puea Thai Party.

0 comments: