UBAKAJI WAKITHIRI : RIPOTI

0
Takwimu za jeshi la polisi nchini Tanzania zinaonyesha kuwa kati ya wasichana kumi wenye umri wa chini ya miaka 18, watatu wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo kubakwa.

Akifungua mafunzo ya namna ya kukabiliana na vitendo hivyo kwa maafisa wakuu wa jeshi la polisi nchini Naibu kamishna wa jeshi la polisi nchini Rashidi Ally amesema kwamba tatizo la ukatili wa kijinsia bado ni kubwa na hivyo linahitaji ushirikiano wa pamoja na wananchi.





Amesema jeshi hilo limekuwa likifanya kazi ya kuhakikisha wa;e wote wanaohusika na vitendo hivyo wanakamatwa na kufikishwa katika mkono wa sheria lakini hayo yote yanategemeana na taarifa kutoka kwa raia wema pale wanapoona mtu anafanya vitendo hivyo.

0 comments: