WATU 9 WAHUSISHWA NA KUMVAMIA DKT MVUNGI.....

0
Idadi ya watuhumiwa waliokamatwa kutokana na tukio la kumjeruhi vibaya mjumbe wa tume ya marekebisho ya katiba Dk. Sengondo Mvungi imeongezeka na kufikia watu tisa baada ya kukamatwa kwa watuhumiwa wengine watatu.




Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dk. Emmanuel Nchimbi pamoja na Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam kamishna Suleiman Kova wamesema watuhumiwa hao watatu wamekamatwa na mapanga matano ambayo yanasadikiwa kutumika kumjeruhi Dk. Mvungi.

Amesema watuhumiwa hao pia wamekutwa na simu moja ya mkononi ambayo inadaiwa kutumika katika mawasiliano kabla ya kufanya tukio hilo, na katika mahojiano na watuhumiwa hao wamebaini kwamba bado kuna wengine ambao watatakiwa kukamatwa kwa ajili ya mahojiano zaidi.


0 comments: