Apotelea Bahari ya Pacific miezi 16...Alikunywa mkojo kuishi...

0
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Mzee moja aliyesadikiwa kupotelea baharini kwa miezi kumi na sita, sasa amerejea nchini kavu, kukiwa na maswali mengi ikiwa iliwezaji kuishi katika mtumbwi wake mdogo kwa muda wote huo, huku kukikwa na hali tete bahari ya Pasifiki?

Mwanaume huyu anayejiita Jose Salvador Alvarenga alitokea katika visiwa vilivyojificha vya Marshall huko Mexico akiwa na mtumbwi wake ulioharibika, akisema kuwa alikuwa akiishi kwa kutegemea samaki na wanyama wengine wa bahari pamoja na kunywa maji ya mvua na wakati mwingine mkojo wake mwenyewe. Alikuwa na kijana mwingine ambaye alifariki kwani alikataa kula ndege na sasmaki wabichi na hakuweza kunywa mkojo wake.

Bado mamlaka nchini humo zinafanya jitihada kufahamu ukweli wowote juu ya hadithi ya bwana Alvarenga. Serikali ya Mexico imetoa tamko kuthibitisha kuwa Bw. Alvarenga ni mwananchi wa El Salvador.

Familia ya Bwana huyu ilipotafutwa ilikiri haijawasiliana naye kwa muda mrefu sana na walidhani pengine alikwisha fariki. Bw. Alvarenga ana mtoto wa kike mweye umri wa miaka 12 ambaye hamkumbuki baba yake.


Hali tete iliyopo katika bahari ya Pasifiki inafanya hadithi ya bwanahuyu kuonekana ni ya kusadikika. Hata hivyo mawimbi yngeweza kuibeba boti hiyo kwa kilometa 42 kwa siku kutoka Mexico mpaka visiwa vya Marshall. Hivyo kutokana na wataalam hadithi yake inaweza kuwa ya kweli.

0 comments: