Bensouda Akalia Kuti Kavu ICC kesho...Zama Humu

0
Rais wa Kenya  Uhuru  Kenyatta
Majaji katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya kihalifu ICC kesho watafanya maamuzi iwapo kesi ya Rais wa nchini Kenya Uhuru Kenyatta itafutiliwa mbali au kuwapa mud azaidi upande wa wachitaki kutafuta ushahidi zaidi.

Maamuzi hayo yatafanyika mkutano maalum ambapo wanasheria wa Rais Kenyatta watafanya jitihada za kutaka kumalizika kwa kesi hiyo, hata hivyo Rais Kenyatta hatahitajika kusafiri kwenda The Hague kwa ajili ya mkutanio huo.

Wakati huohuo, upande wa mashtaka unaoongozwa na mwana mama Fatou Bensouda utatafuta muda zaidi wa kupata ushahidi mpya na mashahizi wengine, baada ya kuripotiw akuwa mashahidi wengine walijiondoa katika kesi hiyo.

Bi. Fatou Bensouda
Bi Bensouda anapinga kufutiliwa mbali kwa kesi ya Bw. Kenyatta na ameituhumu serikali ya Kenya kwa kwa kutoupa ushiriakiano upande wake katika uendeshwaji wa kesi hiyo. Kesi ilipangwa kuanza kusikilizwa tena hiyo kesho.

Upande wa utetezi wa Bw. Kenyatta unaoongozwa na Bw.Mr Stephen Kay, mapema mweziwa kwanza mnamo tarehe 3, uliitaka mahakam kufutia mbali kesi ya Rais Kenyatta kwani ilikuw awazi mno kwamba upande wa mashtaka haukuwa na ushahidi wa kutosha.
Rais Uhuru Kenyatta
Katika majibu yake Bi. Fatou Bensouda aliwaomb amajaji kutupilia mbali ombi hilo. Alisema angehitaji kwanza majaji hao waweke shauri lake lililolalamikia ushirikiano mbovu wa serikali ya Kenya katika uendeshwaji wa kesi hio ambao ulikuwa ukikiuka Mkataba wa Roma yaani ( The Rome statute)

Bi bensoud aalisistiza kuwa, kwa kuwa Kenyatta ndiye Rais wa Kenya anauwezo wa kushinikiza lolote analotaka lifanyike nchini humo. Mahojiiano ya mkutano huo wa kesho yanazidi kuwa ya moto kwa kuzingatia matakwa yaliyopendekezwa na Umoja wa Afrika, ulioiambia ICC, kuwa endapo watashindwa kufanya yale umoja huo unayoyataka basi nchi za Afrika zitajitoa ICC kufikia tarehe 30 ya mwezi wa nne mwaka huu.

Katika barua hiyo iliyoandikwa Tarehe 29 mwezi wa kwanza AU imeainisha vitu kadhaa vinavyotakiwa kushughulikiwa. Kama vileutaalamu udhihirike katika kutafuta mashahidi na kufanya uchunguzi, na pia mahakam iache au kusitisha kupokea fedha kutoka kw awahisani wanaowez kushinika mwenedno wa kesi. AU imeitaka mahakam hii kutoa mpango mkakati watakao utumia kurekebisha haya kufikia mwisho wa mwezi wa wanne

Kumbuka mvutano baina ya nchi zilizoegema Ufaransa na zile za Uingereza unaweza ukawa na nguvu katika mvutano huu wa ICC. Utambue Nchi za karibu na Ufaransa (Francophone) countries sio wanachama wa ICC... Kesi karibu nane zilizopo ICC ni za Waafrika..Lakini pia nchini kama Marekani...Unafahamu kuwa yenyewe ilipitisha sheria ya kuwapa kinga watu wake namahakama hiyo..

Unadhani Nchi za Afrika kuwa wanachama au sio wanachama wa ICC kunaiongezea au kuipunguizia ICC kitu gani? Mbona basi Umoja wa Afrika umetoa onyo la aina hii?

0 comments: