SIKU YA SARATANI DUNIANI...ONA TAHADHARI ILIYOTOLEWA

0
Shirika la Afya duniani WHO limeonya kuhusu kuibuka kwa wimbi baya la maambukizi ya ugonjwa hatari wa saratani kote duniani. Shirika hilo limesema nusu ya maambukizi ya saratani yanaweza kuzuiwa na kwamba juhudi mpya zinastahili kufanyika ili kukabiliana na tatizo la kunenepa kupita kiasi, ulevi na uvutaji sigara.

Watu milioni kumi na nne wanajulishwa kuwa wanaugua saratani kila mwaka, lakini idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka na kufikia milioni ishirini na nne katika kipindi cha miongo miwili ijayo.

Taasisi ya utafiti wa kimataifa kuhusu ugonjwa wa saratani katika shirika la WHO lilionya kuwa gharama ya matimabu inaongezeka kwa kiwango ambacho ni vigumu kumudu. Taasisi hiyo imesema serikali zinahitajika kutekeleza sheria kali zaidi kuhusu matumizi ya pombe na sukari kama vile kuongeza bei na kukataza matangazo ya kibiashara ya bidhaa hizo.

Wakati huohuo, Wanasayansi wanaamini kuwa unywaji mwingi wa pombe unaweza kuleta hisia zisizo za kawaida mwilini ambazo zinaweza kuiweka ngozi katika hatari zaidi ya kupata Saratani ya ngozi.

Kemikali ya Ethanol inapogeuzwa kuwa “Acetaldehyde” baada ya ulaji wa chakula,kemikali hii yaweza kuiwezesha ngozi kupenyeza miale hata ya jua (UV light).

Watafiti waliofanya ugunduzi huo, nchini Uingereza wanakubali kwamba kuna mambo mengine yanayochangia mtu kupata Saratani ya Ngozi.

Sarah Williams wa Utafiti wa Kansa, Uingereza alisema ''Utafiti umeonyesha kuwa wagonjwa wanaougua Melanoma huathirika kwa ajili ya kuota jua kwa muda mrefu,hili linaweza kupunguzwa iwapo mtu atajikinga kutokana na jua kali. Kulingana na utafiti wao uliochunguza mada 16 tofauti na kushirikisha maelfu ya watu,unywaji wa chupa moja ya pombe moja au zaidi kila siku huongeza uwezekano wa kupata Saratani ya ngozi kwa asilimia ishirini.

0 comments: