DOLA MILL. 54 ZAIBWA LIBYA KWA SILAHA

0
Shirika la habari nchini Libya limeripoti kuwa watu wenye silaha wameiba kiasi cha dola milioni 54 katika shambulio la basi dogo lililokuwa limebeba fedha za nchi hiyo na za kigeni za benki kuu ya Libya.

Wanaume hao kumi walilisimamisha basi hilo dogo wakati likiingia katika mji wa Sirte kutoka Uwanja wa ndege ambapo fedha hizo zilisafirishwa kilomita 500 kutoka mji mkuu wa Tripoli.
  

Serikali ya Libya imekuwa ikifanya jitihada za kudhibiti uhalifu katika nchi hiyo iliyojaa vikundi vya wapiganaji wenye silaha, wahalifu na waislamu wenye msimamo mkali.

0 comments: