M23 SASA WAFIKA KIAMA

0
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo ameliambia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa waasi wa M23 ni kama wamedhibitiwa kabisa na si tishio tena.

Mjumbe huyo Martin Kobler amesema waasi wa M23 wameng'olewa katika ngome yao kuu ya Rutshuru na kwa sasa wamejikusanya wakiwa kundi dogo karibu na mpaka wa Rwanda.


Ngome hiyo ni ya tano kutwaliwa na vikosi vya serikali katika mapambano yaliyodumu kwa wiki moja yaliyowasambaratisha waasi hao wa M23. Hata hivyo waasi wamesema kuachia ngome zao hizo ni kwa muda tu.

0 comments: