FUATILIA UCHAMBUZI YAKINIFU WA HOTUBA YA RAIS OBAMA HAPA...
0
Akitumia maneno na mifano ya kawaida kabisa, yake ya Barack Obama hapo jana ametoa hotuba ya mwaka nchini Marekani hotuba ambayo husikilizwa na kutiliwa maanani pengine zaidi ya nyingine. Katika hali ya kutaka kupunguza makali ya propaganda za kiasiasa zinazoendelea kumjeruhi Rais huyu mashuhuri, Bw. Obama ameita mwaka huu kuwa ni mwaka wa Vitendo, ambapo amesema atafanyakazi na wanasheria ikiwa ni sehemu ya kutafuta ahueni ya maisha kwa familia za kipato cha kati na cha chini.
Katika
hotuba yake hii iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu, Rais Obama ameahidi
kutumia madaraka yake kuongeza mishahara kwa wafanyakazi, kulinda
mazingira ya kufanya kazi hasa kwa wanawake na pia kuelekeza
rasilimali zaidi kwa elimu hasa ya msingi.
Swala
la Afya lazima hutokea katika hotuba za Rais Obama. Hasa ukizingatia
umuhimu wa kusukuma agenda yake ya Obamacare, mradi ambao bado
haujaonesha mafanikio ya kutosha.
Hotuba
hii ya Rais Obama imekuja wakati ambapo kura za kutathmini utendaji
wake hazikurudhisha. Hii inaleta hofu kubwa kuwa huenda katika
chaguzi za useneta mnamo mwezi wa 11, chama cha Democrat kinaweza
kupoteza nafasi nyingi. Hivyo
miezi hii michache ni ya Rais Obama kufanya kila awezalo,
kuwashawishi wamarekani katika sera za kiuchumi ilikurudisha imani ya
wengi iliyotoweka.
Obama
ameliambia bunge la Marekani “The congress” wazi kuwa sio lazima
wamruhusu afanye kila kitu au sio lazima apitishe agenda zake zote
kwao, lakini anaweza pia kufanya yeye mwenyewe.
Kwa
upande mwingine Obama alijibiwa hotuba yake hiyo na mwanamama Cathy
McMorris ambaye aliuwakilisha upinzani. Japokuwa Republicans hawalipi
swala la usawa katika ajenda zao kwa kuwa wote ni mabepari,
walionekana kukubaliana na hilo jana.
Hata
hivyo, kutangazwa kwa kima cha chini kwa Rais Obama ilikuwa ni mfano
tosha wa mipango yake ya kufanya maamuzi bnila kulishirikisha bunge,
japo haijulikani Rais Obama ataweza kufanya hivi kwa muda gani
Kima
hichi kitapanda kutoka dola 7.25 kwa saa mpaka dola 10 kwa saa.
Ongezeko
hili litaathiri sana watoa huduma kama vile wale wa migahwa mn awa
vyombo vya usafiri hivyo kufanya pato la mfanyakazi aliyeajiriw akw
amwak akufikia Dola 21,000 kutoka dola 15,000
Tumemzoea
akitumia maneno na mifano ya kawaida kabisa kuelezea mambo magumu na
yanayoamua mustakabali wa nchi ya Marekani na dunia kwa ujumla.
Unadhani mtindo huu wa Obama unamfanya atofautian ana wanasiasa
wengine duniani? Na je unaonaje wanasiasa wengine wakiiga mfano wake?
NB:TOA MAONI YAKO