Ona Wachina walichofanyiziwa siku ya Valentines....Hapa

0
Baadhi ya wapenzi nchini China leo watakosa fursa ya kukaa kiti kimoja wakati wakuangalia filamu katika Siku ya Wapendanao, kutokana na kampeni ya kuwatenganisha iliyoanzishwa na mwanaume mmoja asiye na mpenzi.

Mwanaume huyo ambaye jina lake halijajulikana amekuwa akinunua tiketi ya kiti kimoja katika kila viti viwili za jumba kuu la sinema la Shanghai, ili kuwadhibiti wapenzi wasikae pamoja kampeni ambayo pia iliungwa mkono na
watu wasio na wenza nao kununua tiketi kwa mtindo huo.

Siku ya Wapendano nchini China hutumika kwa kuangalia filamu maalum inayoonyesha historia ya mapenzi katika Mji wa Beijing.

Mwanaume huyo amesema kitendo hicho alichofanya cha kuwadhibiti wapendano kukaa pamoja kuangalia filamu hiyo ni mzaha tu na anatarajia wapendanao watamuelewa.
 

0 comments: