7 WAFARIKI DUNIA LEO KATIKA AJALI MIOROGORO

0
Watu saba wamefariki dunia papo hapo leo asubuhi na wengine watano wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wanasafiria aina ya Noah kugongana uso kwa uso na lori la mizigo maeneo ya Dakawa mkoani Morogoro.



Akithibitiha kutoka kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile amesema ajali hiyo imetokea baada ya Noah kujaribu kulipita gari hilo ndipo lilipogongana uso kwa uso na Lori ambapo watu waliopoteza maisha walikuwa kwenye Noah.


Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Anthony Mtaka akizungumza kutoka kwenye eneo la tukio amewataka madereva kufuata sheria za barabarani ili kuepusha ajali kama hizo zisizokuwa za lazima zinazogharimu maisha ya watu pamoja na mali.



0 comments: