MINYOO WATUMIKA KUANDAA DAMU BANDIA

0
MINYOO WA BAHARINI WANAWEZA KUTUMIKA KUTENGENEZA DAMU BANDIA KWA AJILI YA MAJERUHI WANAOHITAJI AU WALIOPOTEZA DAMU NYINGI....
Wanasayansi wa nchi ya Romania wamesema wanaweza kuwa njiani kukamilisha matayarisho ya damu BANDIA lakini salama na ya kuaminika kwa matumizi ya binadanmu HASA KATIKA kuokoa maisha ya watu waliopata majeraha na kupoteza damu nyingi.... Watafiti kwa miaka mingi wamekuwa wakijaribu kutengeza chembechembe nyekundu za damu (HAEMOGLOBIN ) BANDIA itakayoweza kubeba hewa ya Oxygen mwilini bila mafanikio. Hata hivyo wanasayansi hwa wa Romania wamedai kuwa vipimo na majaribio walioyafanya kw akutumia hemerythrin, chembechembe zilizotokana na minyoo wa baharini wanona dalili ya kufaulu katik aswala hili.
Utafiti huu umezua utata baada ya kubadilika kwa damu hii pale inapokutana na kemikali nyingine...Hata hivyo Prof rossi solagidumitresco na Timu yake katika chuo cha Bandesi Buyahi amesem akuwa damu hii ilipojaribi wakw apanya haikuleta maafa yoyote.

…..Prof...Damu hii haifungamani sana na kemikali nyingine kwenye damu...ambazo kemikali hizi huiharibu haemoglobini ndani ya sekunde..Lakini hii haiharibiki haraka kiasi hicho...

Damu hii bandia inatengenezwa na maji na chumvi pamoja na kemikali maalum. Badala ya kuwa nyekundu kama ilivyo damu ya kawaida hii hutengeza mchanganyiko wa Njano kwa mbali..Timu hii inaamini kuwa uvumbuzi huu unaweza kuleta mapinduzi katika tasnia ya afya...Kama wanavyoonesha Protini maalum ya kusafirisha damu kwa wanyama wasio na uti kama wajulikanao kama Invertebrates..inawezesha pia kutumika kwa walionao wanajulikana kama Vertebrates hivyo Panya walitumiwa. Ili kuhakikisha kuwa kemikali hii ni thabiti na haiwezi kubadilishwa na kemikali zozote au chembechembe mwilini, inaweza kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika..

Prof:...Kama damu ya binadamu inaweza kukaa katika friji kwa miezi na baadae kutupwa kwa kuharibika..hii tunaweza kuiweka kwenye kabati au tukasafiri nayo...na tukiichanganya na maji safi..tunapata Damu hapohapo...
Watafiti hawa wanaamini kuwa damu hii inaweza kutuimika kwa wagonjwa wakliopo njiani kuelekea hospitalini au hata vitani ambapo hospitali haipo karibu...Wanaendelea kufanya majaribio yao kwa Panya na ndani ya Miaka 2 wataweza kuanza kufanya majaribio kwa Binadamu....

0 comments: