PAKA ATISHA POLISI KWA SIMUU...IONE HII...

0
Mapolisi katika eneo moja jijini London, nchini Uingereza walishtushwa na kwenda mara moja eneo la tukio baada ya simu ya hatari kupigwa bila ya kuwa na mzungumzaji yoyote kwa upande wa aliyepiga.

Mapolisi hawa walipokimbia wakidhani huenda aliyekumbwa na tatizo hilo yupo katika hali mbaya, wakiwa kwa nje ya nyumba hiyo walisikia kelele za kuparuana, ndipo walipovunja mlango wa nyumba hiyo na kushangazwa kumkuta paka aliyejulikana kwa jina la Bruce akicheza na paka mwenzake katika gorofa hiyo aliyejulikana kwa jina la Audrey.

Paka huyu alikuwa nyumbani, walezi wake walipokwenda kazini na huenda alikua akitafuta kujaliwa kidogo yaan “he was seeking attention”. 


Hata hivyo Poilisi waliwataka wamiliki wa Paka hao kueleza kilichotokea. Ambapo ilielezwa kuwa Paka wake hukimbilia simu inapoita na anapenda kuchezea vibonyezo vya simu hiyo. Mmiliki huyu amelazimika kutumia kiasi cha Paundi 100 Takriban Shs. Laki 2 kw aajili ya kuurekebisha mlango wake... Upo apo...



0 comments: