MFAHAMU ZAIDI ARIEL SHARON..UNAJUA ALIOA MTU NA DADA YAKE?

0
Maelfu ya Waizraeli hapo jana walitoa salamu zao za mwisho kwa mpendwa wao, kiongozi wao na aliyekuwa waziri mkuu mstaafu Hayati Ariel Sharon hapo jana mwili wake ulipowekwa nje ya jengo la bunge la Israel.

Mambo machache usiyafahamu kuhusu Sharon. Ariel Sharon alizaliwa tarehe ya 26 mwezi wa pili....1928. Alikuwa muisraeli na jenerali katika kikosi cha jeshi cha nchi hiyo. Alitumikia Israel kama waziri mkuu wa 11 mpaka alipopatwa na ugonjwa wa kiharusi uliomfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake ipasavyo hivyo kuachia ngazi.

Alikuwa kamanda wa kikosi cha jeshi cha Israeli kwanzia mwaka 1948.

Sharon ambaye alibatizwa jina la Man of Action


yaani mtu wa vitendo... amewahi kuwa mjane mara mbili. Alioa mke wake wa kwanza Margalit baada ya kuwa kiongozi wa kikosi ambaye walipata mtoto mmoja. Lakini Margalit alifariki dunia mwaka 1962 baada ya kupata ajali ya gari. Mtoto wao Gur alifariki mwaka 1967 baada ya kupigwa risasi na rafiki yake ambaye walikuwa wakicheza kama watoto kwa kutumia bunduki. Baadaye Ariel Sharon alimuoa mdogo wa mkewe wa Kwanza aliyeitwa Lily. Lily alikuwa mrembo sana. Walipata watoto wawili Omri and Gilad. Kwa bahati mbaya sana Lily naye alifariki dunia mwaka 2000 baada ya kupata ugonjwa wa saratani ya Mapafu.


Mamia walisikka wakisifia uwezo wake mkubwa kijeshi na kwamba ni kati ya viongozi wachache waliojitoa kufa na kupona kupigania nchi yao.

Ariel Sharon aliyefariki jumamosi iliyopita baada ya kukaa katika hali ya kutojitambua yaani Coma kwa takriban miaka nane amesababisha majonzi makubwa kupita kiasi nchini Israel. Sharon ataagwa tena leo kiserikali na kuzikwa katika hafla itakayoshuhudiwa na Viongozi wa kidumia kama Naibu Rais wa Marekani Joe Biden na aliyekuw awaziri mkuu wa Uingereza Tony Blair.

Shughuli hii itaanzia Latrun kutakapokuwa na mkutano wa viongozi wa kijeshi kabla ya mwili wa Sharon kupelekwa shambani kwa Sharon Shikmim kwa ajili ya maziko. Waziri mkuu Wa Israel wa sasa Benjamin Netanyahu amemuelezea Sharon kwa kiongozi mzuri wa kiasiasa na kinara wa vita.

Hata hivyo watu wengine wametoa sifa mbaya kwa Sharon hasa wakazi wa Ukanda wa Gaza na Palestina. Maamuzi yaleyale yaliyomfanya Sharon kiongozi mtata wakati wa uongozi wake mrefu kama kongozi wa Jeshi na mwanasiasa yalionekana tena pale tu alipofariki.

Hii inajumuisha kuwa kwake waziri wa Ulinzi manmo mwaka 1982 katika vita ya Lebanon. Wakati huo Sharon alishikiliwa kama muhusika mkuu katika vifo vya maelfu ya watu waki Palestina katika kambi za wakimbizi za Sabra Shatila. Alilazimishwa kujiuzulu.


Aliwahi kusababisha adha kubwa pale alipowaamuru waisraeli wajenge katika ardhi iliyosemekana ni ya wa Palestina na baadae kugeuka ghafla na kuwarudishia wapalestina ardhi yao kwa mara ya kwanza katika miongo minne. Rais wa Israel Shimon Peres alitoa hotuba kwa ajili ya Sharon akimuita rafiki Arik Sharon jina ambalo ni la utani kwa Sharon. Alimtaja kama mtu aliyetukuka aliyewapenda watu wake an watu wake wakampenda zaidi.

Tunasema Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake liimidiwe.
Watu mashuhuri na vinara wa nchi zao wanapofariki, kunakuwa na hali za kufana katika nchi tofauti tofauti...Je unafahamu zi zipi hizo...Tafadhali toa maoni yako...

0 comments: